ARTICAL



 HISTORIA YA TATA NELSON MANDELA, ALIYE GEUZA HISTORIA YA DUNIA KWA KUITWA GAIDI NA BAADAE AKAITWA SHUJAA NA MWAMBA WA AFRIKA................TATA MADIBA
                                      

 
Tanzia: Nelson Rolihlahla Mandela
BABA wa Demokrasia ya Afrika Kusini, Mzee Nelson Rolihlahla Mandela ambaye alizikwa Jumapili iliyopita, Desemba 15, 2013 katika kijiji cha asili ya familia ya akina Mandela cha Qunu, nje kidogo ya mji wa Mthatha, Jimbo la Cape Mashariki (Eastern Cape) aliaga dunia Alhamisi ya Desemba 5, mwaka huu, saa mbili na dakika 50 za usiku akiwa amezungukwa na familia yake nyumbani kwake mjini Johannesburg akiwa na umri wa miaka 95.

Mandela ambaye alikuja kutokea kuwa taa ya uhuru, demokrasia na haki duniani, alizaliwa katika Kijiji cha Mvezo, kiasi cha kilomita 30 kutoka Qunu katika eneo la Transkei Julai 18, mwaka 1918, mama yake akiwa Nongaphi Nosekeni na baba akiwa Henry Gadia Mandela.

Baba yake alikuwa mshauri mkuu wa Nyumba ya Kifalme ya Thembu na baada ya kifo chake mwaka 1927, Rolihlahia akiwa bado mtoto mdogo wa miaka tisa, alichukuliwa na kupewa nafasi ya Chief Jongintaba Dalindyebo, mtawala wa muda wa taifa la Thembu. Ilikuwa kwenye Nyumba hiyo ya Kifalme ambako utu wake, imani yake, thamani zake katika maisha na misimamo yake ya kisiasa vilianza kujengeka. Hivyo basi siyo jambo la kushangaza kuwa kijana huyo mdogo alikuja kutokea kuleta mageuzi makubwa na ya msingi katika historia na siasa za Afrika Kusini.

Ilikuwa ni kupitia kwa Mandela kwamba dunia ilikuja kuijua Afrika Kusini na kuanza kugundua na kujua ugandamiza na unyanyasaji mkubwa wa Waafrika katika Afrika Kusini. Na baadaye ilikuwa kupitia kwa Mandela kuwa dunia ilikuja kujifunza na kujua moyo wa uvumilivu, ushindi wa kusameheana na uzuri wa maridhiano katika maisha ya binadamu na maisha ya kisiasa.

Alikuwa bado na umri mdogo wa miaka 25, mwaka 1942, alipojiunga na Chama cha Ukombozi wa Afrika Kusini cha African National Congress (ANC). Na tokea siku hiyo, maisha yake ya kisiasa yamekuwa ya kudumu kwa miongo mingi. Kama alivyopata kusema mwenyewe, “Mapambano ndiyo maisha yangu.”

Akiwa kijana, Mandela alisomea, akafaulu na kufanya kazi kama mwanasheria. Yeye na rafiki yake wa karibu ambaye alikuja kuongoza ANC kwa miaka mingi wakati Mandela akiwa jela, Oliver R Tambo, walifungua kampuni ya kwanza ya sheria iliyomilikiwa na Waafrika mjini Johannesburg.

Mandela alimwoa Evelyn Nomathamsanga Mase mwaka 1945. Walioana kwa miaka 14 na kupata watoto wanne: Thembekile aliyezaliwa mwaka 1946, Makaziwe (1947) ambaye alipoteza maisha akiwa bado na miezi tisa tu, Makgatho (1951) na Makaziwe (1954) binti mkubwa wa Mandela na mtoto aliyebakia kutokana na ndoa yake ya kwanza. Mandela na Evelyn walitalikiana mwaka 1958.

Mandela alitoa mchango mkubwa katika kuanzishwa kwa Kikundi cha Vijana wa ANC cha ANC Youth League (ANCYL) chenye msimamo mkali katika miaka ya 1940. ANCYL kilidhamiria kubadilisha kabisa sura na mwenendo wa siasa za Afrika Kusini na za chama cha ANC chenyewe. Mandela alichaguliwa kuwa Katibu Mkuu wa kwanza wa taifa wa ANCYL mwaka 1948 na mwaka 1952 alichaguliwa kuwa Rais wake.

Kwa miaka mingi iliyofuatia ilimshuhudia Mandela alishiriki kwa undani kabisa katika uanaharakati wa kisiasa, akiwa anahamasisha mabadiliko ya kisiasa dhidi ya utawala wa Makaburu ambao ulikuwa nao umeongeza kasi ya ukatili dhidi ya Waafrika. Mandela alikuwa mtu muhimu sana katika Kampeni ya ANC kupinga sheria kandamizi ya Campaign for the Defiance of Unjust Laws mwaka 1952 na katika Kesi ya Uhaini ya Rivonia mwaka 1961.

Katika kipindi hicho alikamatwa na kuwekwa ndani mara kadhaa chini ya Sheria za Kikaburu na alipigwa marufuku kushiriki katika harakati za kisiasa.

Akijua fika kuwa ANC ilikuwa inahitaji maandalizi ya aina tofauti na yenye ari na kasi zaidi, Mandela alikuwa mmoja wa waanzilishi wa mapambano ya silaha ya ukombozi kwa kuunda Jeshi la ANC la Umkhoto we Sizwe (MK). Jeshi hili liliundwa kwa madhumuni makuu ya kuandaa mapambano ya silaha na Mandela alikuwa Amiri Jeshi wake mkuu wa kwanza.

Juni 14, mwaka 1958, Nelson na Winnie Madikizela walifunga pingu za maisha katika kanisa moja dogo la Bizana. Walijaliwa watoto wawili – Zenani (1958) na Zindziswa (1960). Aprili 1992 walitengana na hatimaye kutalikiana kabisa mwaka 1996.

Mandela aliondoka Afrika Kusini mwanzoni mwa mwaka 1962 kwenda nchi za nje kutafuta sehemu za kuwafundisha mbinu za kivita wana-MK. Nchi ya kwanza kutembelea ilikuwa Tanzania baada ya kuwa amesafiri kwa mbinu za kila aina kupitia katika nchi za Bechuanaland (Botswana) na Northern Rhodesia (Zambia) bila hati ya kusafiria. 
 
Ilikuwa katika Tanzania ambako alikutana na Baba wa Taifa, Mwalimu Nyerere, ambaye alikubali kuwafundisha kijeshi wapigania uhuru wa MK na kupata nyaraka za kusafiri kwenda nchi za Ghana, Nigeria, Algeria na Ethiopia.
Aliporudi tu Afrika Kusini, Mandela alikamatwa kwa kuondoka nchini kinyume cha sheria na kwa kushiriki katika uchochezi wa kutaka wafanyakazi wagome dhidi ya Utawala wa Kikaburu. Ipoanza kesi, Mandela aliongezewa shitaka jingine la kushiriki hujuma. Mandela aliamua kujitetea mwenyewe mahakamani.

Ilipoanza kesi hiyo iliyojulikana kwa umaarufu wa Rivonia Trial, Mandela aliotoa kauli iliyokuja kuwa maarufu sana hata kama ilitolewa miaka mingi iliyopita, mwaka 1964. Alisema Mandela: 
 
Nimepambana na kupigana dhidi ya utawala wa mabavu na kidhalimu wa Kizungu na pia nimepambana na kupigana dhidi ya utawala wa mabavu na kidhalimu wa Kiafrika. Nimeamini kwa muda mrefu katika jamii ya kidemokrasia na huru ambako watu wote wanaishi kwa pamoja na kwa amani na kuwa na fursa sawa. Ni imani ambayo nataraji kuishi na kuiona ikipatikana. Lakini kama ni lazima ni imani ambayo niko tayari kuifia.”

Ilikuwa mwaka huo Mandela na wenzake kwenye kesi hiyo ya Rivonia walipohukumiwa kifungo cha maisha na kupelekwa jela kwenye Kisiwa cha Robben, karibu na mji wa Cape Town.

Akiwa jela, Mandela alikataa ofa kadhaa za waliomfunga za kuachiwa huru kwa masharti kuwa anakana hadharani matumizi ya nguvu katika kudai haki ya wote na hasa Waafrika waliokuwa wanakandamizwa.

Kila alipopewa ofa hiyo, Mandela aliwakumbusha waliomfunga: “Wafungwa hawawezi kuingia katika makubaliano yoyote ya kisheria. Ni watu huru tu wanaoweza kujadiliana na mwenzao.” Alitumikkia miaka 27 jela kwa imani yake ya kupambana na siasa za Ubaguzi wa Rangi na udhalimu wake wote.

Mandela aliachiwa huru Februari 11, mwaka 1990, na mara moja akajitumbukiza katika shughuli yake ya maisha akijaribu kufanikisha malengo ambayo yeye na mwenzake walikuwa wamejiwekea miongo mine kabla ya kabla ya hapo. 
 
Mwaka 1991 katika Mkutano Mkuu wa kwanza wa ANC kufanyika ndani ya Afrika Kusini yenyewe baada ya chama hicho kupigwa marufuku kwa miongo mingi, Nelson Mandela alichaguliwa Rais wa chama hicho wakati rafiki yake wa maisha, Oliver Tambo alichaguliwa kuwa Mwenyekiti wa Taifa wa ANC.

Katika maisha ambayo yanaashiria ushindi wa roho ya binadamu, Nelson Mandela alikubali kupokea Tuzo ya Amani ya Nobel pamoja na Kiongozi wa Makaburu aliyemwachia huru, FW de Klerk kwa niaba ya wananchi wote wa Afrika Kusini ambao waliteseka na kuhangaika sana kuleta amani katika Afrika Kusini.

Utawala na kipindi cha Ukaburu kilifikia mwosho rasmi Aprili 27, 1994, wakati Nelson Mandela alipopiga kura kwa mara ya kwanza katika maisha yake – pamoja na watu wake. Lakini siku nyingi kabla ya siku hiyo, ilikuwa imekuwa dhahiri, hata kabla ya mazungumzo ya Afrika Kusini mpya katika Ukumbi wa World Trade Centre, Kempton Park, kuwa ANC ilikuwa imekamata uongozi wa maisha ya baadaye ya Afrika Kusini na wananchi wake.
Nelson Rolihlahla Mandela aliapishwa kuwa Rais wa Afrika Kusini yenye demokrasia Mei 10, mwaka 1994.

Mandela alifanya kazi usiku na mchana bila kuchoka kuboresha maisha ya wananchi hata baada ya kufanikisha kupatikana kwa demokrasia katika Afrika Kusini. Hata baada ya kustaafu kutoka siasa, alielekeza nguvu zake kwenye masuala ya kijamii kama mapambano dhidi ya ukimwi na ubora wa maisha ya watoto wa Afrika Kusini.
Bwana Mandela ameacha mjane, Graca, watoto watatu wa kike, wajukuu 18 na vitukuu 12.
 
 ************************************************** ************************************************* *******************************

KITENGO CHA MADAWA YA KULEVYA HAPA NCHINI TUNAOMBA MAJIBU JUU YA BARUA HII YA MSAFIRISHAJI WA MADAWA YA KULEVYA............


Barua iliyo muhusisha Mbunge wa Kinondoni Mhe Idd Azan na biashara ya madawa ya kulevya
( Aijadhibitishwa kama ni kweli )








Kwa muda sasa kumekuwa na matukio ya watanzania kukamatwa kwa tuuma za madawa ya kulevya huku serikali ikikaa kimya ilikuonyesha kutokujua juu ya biashara haramu za dawa za kulevya na kukazia mamcho biashara ya Gongo tu....

Pia Wasanii wetu wamehusika katika mengi yanayo ihusisha tasnia hiyo na biashara hiyo japo si wote, Hivisasa barua inayomhusisha Mhe. Idd Azan na biashara za madawa ya kulevya tuhumba ambazo azija dhibitishwa mpaka sasa

Maajabu ya Barua hiyo kwangi ni kwamba, Kwa nini mwandishi kamtaja Idd Azan na kuwaacha wengine kama kweli vigogo wengi wanahusika na anawajua na anajutia kosa na yuko tayari kueleza ukweli....Je anaugomvi naye au nimfano wa wengine? kwanini asinge wataja wote, 

kuna baadhi ya wafanya biashara wakubwa kawataja kwa majina na mahali wanapo kaa pamoja na biashara zao je Mbona akusema majina ya wafungwa wenzake...hayo ni mawazo yangu lakini hawa hapa chini watakuwa wanamajibu au wanajua pakuanzia japo kua hakuna ambaye yuko tayari kusema ukweli .....................


KITENGO CHA MADAWA YA KULEVYA NDANI YA JESHI LA POLISI MTUPE MAJIBU YAHAYA YOTE KAMA NIUKWELI AU SIKWELI, HIZO NJIA ZILIZO TAJWA HAPA ZINAZO TUMIKA KWAAJILI YA KUINGIZA BIDHAA HIZO HAPA NCHINI MNAZIFAHAMU? NA WAHUSIKA WANAHUSIHWA KIUKWELI AU? KAZI HII MNAIWEZA SANA TUNAOMBA MAJIBU...... 


***************************************************************************************


       WATUNISHA MISULI INAWAHUSU

Muscle man

Scientists have discovered a new truth behind big muscles, turning 50 years of knowledge on its head.
Bulging biceps get their power from a mesh arrangement of cells rather than long ropes, detailed studies reveal.
As muscles flex, tugging filaments fan out in a lattice, say the University of Washington team who made the breakthrough.
This generates force in multiple directions, not just up and down the muscle, Proceedings B journal reports.

Start Quote

This aspect of muscle force generation has flown under the radar for decades and is now becoming a critical feature of our understanding of normal and pathological aspects of muscle”
Researcher Prof Thomas Daniel
And it's not just biceps that use this force - all muscles, including the heart appear to do it.
Muscle mesh

Start Quote

This aspect of muscle force generation has flown under the radar for decades and is now becoming a critical feature of our understanding of normal and pathological aspects of muscle”
Researcher Prof Thomas Daniel
And it's not just biceps that use this force - all muscles, including the heart appear to do it.
Prof Thomas Daniel, one of the researchers, said: "This aspect of muscle force generation has flown under the radar for decades and is now becoming a critical feature of our understanding of normal and pathological aspects of muscle."
The basics of how muscle generates power remain the same - filaments of myosin tug on filaments of actin to shorten or contract the muscle.
But myosin doesn't tug in one direction, as previously thought. Instead, it pulls at angles and this gives radial force.
The news will be of interest to bodybuilders who strive to max their muscle power, but could also help doctors treating heart problems.
Co-author Michael Regnier said: "In the heart especially, because the muscle surrounds the chambers that fill with blood, being able to account for forces that are generated in several directions during muscle contraction allows for much more accurate and realistic study of how pressure is generated to eject blood from the heart.
"The radial and long axis forces that are generated may be differentially compromised in cardiac diseases and these new, detailed models allow this to be studied at a molecular level for the first time."

*********************************************************************************

Amazing Facts About The Air Force One (official ‘plane’ Of The US President) 



Air Force Once the Large Plane i never see before...... until Obama Visit Tanzania

1."Air Force One" isn't technically a plane: It's simply the radio call name for any U.S. Air Force plane carrying the president of the United States. As soon as the president steps aboard an Air Force plane, that plane is referred to as Air Force One by the crew and all air traffic controllers, in order to avoid confusion with any other planes in the area. If the president rides on an Army aircraft, that aircraft is Army One, and whenever he boards his specialized helicopter, that craft is Marine One. Civilians generally refer to the physical plane itself as Air Force One

2.Today, there are actually two customized Boeing 747-200 B jets that regularly fly under this designation. They are nearly identical and are almost as tall as a six story building, and as long as a city block.

3.Air Force One is one of the most recognizable symbols of the presidency. Emblazoned with the words "United States of America," the American flag, and the Seal of the President of the United States, it is an undeniable presence wherever it flies

4.Air Force One has unlimited range and can carry the President wherever he needs to travel. The onboard electronics are hardened to protect against an electromagnetic pulse, and Air Force One is equipped with advanced secure communications equipment, allowing the aircraft to function as a mobile command center in the event of an attack on the United States. The media refer to it as “The flying Oval Office” or the “ The flying White House”. On September 11th, 2001, the president's plane showed that it was much more than an executive jet -- it became a mobile bunker when all ground positions seemed vulnerable to attack

5.Air force One has four General Electric CF6-80C2B1 jet engines, which provide 56,700 pounds of thrust a piece. The top speed is between 630 and 700 miles (about 1,126km) per hour and the ceiling maximum (i.e how high the plane can fly) is 45,100 feet (commercial 747s fly at about 30,000 feet)

6.The plane carries 53,611 gallons (about 203,000 litres) of fuel and weighs 833,000 pounds (about 377,000 kg) fully loaded for a long-range mission. With a full tank, the plane can fly half way around the world. The plane has mid-ir refueling capability. As with the B-2 and other combat craft, in-flight refueling gives Air Force One the ability to stay up in the air indefinitely, which could be crucial in an emergency situation

7.Inside, the President and his travel companions enjoy 4,000 square feet of floor space on three levels, including an extensive suite for the President that features a large office, lavatory, and conference room. The president has onboard living quarters, with his own bedroom, bathroom, workout room/gym and office space. Air Force One also includes a medical suite that can function as an operating room, and a doctor is permanently on board. The plane’s two food preparation galleys can feed 100 people at a time

8.Air Force One also has quarters for those who accompany the President, including senior advisors, Secret Service officers, traveling press, and other guests. Several cargo planes typically fly ahead of Air Force One to provide the President with services needed in remote locations

9.The two planes are military aircraft, designed to withstand an air attack. Among other things, the plane is outfitted with electronic counter measures (ECM) to jam enemy radar. The plane can also eject flares to throw heat-seeking missiles off course.

10.The plane is completely off limits to Many. Even visiting politicians and journalists aren't allowed in some parts of the plane, and the Air Force is careful to conceal specific details of the craft's layout including its advanced avionics and defenses





11.One of the most remarkable feature on the plane is its extensive electronics. It has 85 onboard telephones, a collection of two-way radios, fax machines and computer connections. It also has 19 televisions and assorted office equipment. The phone system is set up for normal air to ground connections and secure lines. The president and his staff can reach just about anybody in the world while cruising tens of thousands of feet in the air. The onboard electronics include about 238 miles of wiring (twice the amount you'd find in a normal 747). Heavy shielding is tough enough to protect the wiring and crucial electronics from the electromagnetic pulse associated with a nuclear blast

12.Air Force one is a military aircraft, designed to withstand an air attack. Among other things, the plane is outfitted with electronic counter measures (ECM) to jam enemy radar. The plane can also eject flares to throw heat-seeking missiles off course. Some of the most interesting parts of the plane -- its advanced avionics and defenses -- are classified

13.Every Air Force One flight is classified as a military operation, and it is handled as such. Air Force crews at Andrews Air Force Base in Maryland carefully inspect the plane, and the runway, before every flight. When it's time to head off, the Marine One helicopter brings the president from the White House to Andrews Air Force Base. Teams all over the base keep an eye out for any unauthorized craft in the area and are authorized to shoot on sight. In advance of every Air Force One flight, the Air Force crew sends C141 Starlifter cargo carrier planes, toting the president's motorcade, to the destination. This collection of bulletproof limousines and vans, loaded with weaponry, keeps the president safe on the ground.

14.Air Force One can comfortably carry 70 passengers and 26 crew members . These crew members are carefully screened military personnel, with exemplary service histories. Even the crew members who prepare meals must operate with a high level of security. For example, when buying food, they must hit the stores undercover, and they must select markets at random, in order to protect the president from a poison attack. Onboard the plane, the crew provides 24-hour first class service. 

15.Most presidents form close connections with their flight crew, and the final Air Force One flight is always an emotional trip.




***********************************************************************************


hotuba ya waziri mkuu.odt

MAKADIRIO YA  MATUMIZI  YA  FEDHA  YA OFISI  YA  WAZIRI MKUU, OFISI  YA  WAZIRI MKUU - TAWALA  ZA  MIKOA  NA  SERIKALI  ZA MITAA NA OFISI YA BUNGE  YA MWAKA 2013/2014

 MUHTASARI


********************************************************************************

DOMINICAN REPUBLIC- NCHI AMBAYO WANAWAKE WENGI HUISHI KWA KUJIUZA KUTOKANA NA UMASIKINI ULIO KIDHIRI

 Asilimia 87.8% ya watu wazima katika nchi hiyo hawakuhudhuria shule, Asilimia 25% wanakabiliwa na umaskini uliokidhiri na wengi wao wanakaa vijijini na huacha shule wakiwa na umri mdogo

 

***************************************** **********************

THIS DAY IN HISTORY, 28.3.1953

Watson and Crick discover chemical structure of DNA


On this day in 1953, Cambridge University scientists James D. Watson and Frances H.C. Crick announce that they have determined the double-helix structure of DNA, the molecule containing human genes.

DNA- ni chembe zilizopo kwenye mfumo wa kijenetiki kwaajili ya maendeleo na utendaji wa viumbe hai vyote

**************************************

ARNOLD NDANI YA THE LAST STAND 2013


Baada ya kumaliza mudawake wakuwa Gavana wajimbo la Califonia, Anord Schwarzenegger ameanza mwaka na Movie mpya ya 2013 inayoitwa THE LAST STAND,
  
Movie hii ya ACTION staring ni Arnold mwenyewe lakini imeandikwa na ANDREW KNAUER na kuongozwa na KIM JI- WOON, huku producer akiwa ni LERENZO DI BONAVENTURA 






Movie hii inalengo la kuwazuia wauzaji hatari wa madawa ya kulevya ambao walikuwa wanaitaji kutorokea Mexico sasa Arnold anawazuia hawa watu.

Arnold yeye ni kitaaluma ni mtunisha misuli, Muigizaji, Model, Mfanya biashara, Muwekezaji na mwanasia kupitia chama cha Republican na amekuwa Gavana kuanzia 2001 mpaka 2003. yeye ni raia wa Marekani na Mzaliwa wa Autralia.

 
Arnold amezaliwa mwaka 1947. July 30 na hivi sasa anamiaka 65. amejaliwa kuwa na watoto watano. Movie hii mpya inatoa nafasi kwa Arnold kuruditena kwenye ulingo wangumi kama mpiganaji mahiri wa miaka 80's. Tangu anaanza kucheza movie tayari ameshiriki Movie zaidi ya 36 zikiwemo na zile ambazo ametunga yeye mwenyewe

Anord anautajiri wa Dola za kimarekani Millioni 300, baadhi ya mastaer ambao pia wameigiza kwenye Movie hii ni Forest Whitaker, Johnny Knoxville, Rodrigo Santoro, Luis Guzmán, Eduardo Noriega, Peter Stormare, Jaimie Alexander, Zach Gilford and Génesis Rodríguez.

**************************************************************

  REKODI ZA MESSI, RONALDO NA INIESTA HIZI HAPA

    NANI KUIBUKA MCHEZANI BORA WA DUNIA 2012

Posted on: 7.1.2013

By; Loyce Joseph

*******************************************************

 HISTORIA FUPI YA MAREHEMU SAJUKI

Kaka wa marehemu Salum Kilowoko amesema kwamba, Marehemu alizaliwa April 14 1986 na kuanza elimu ya msingi mwaka 1994 katika shule ya msingi Sokoine na kuhitimu mwaka 2000. na kwamba wao ni wangoni kwa kabila ambao wanapatikana kusini mwa Tanzania yani mkoa wa Songea

“Marehemu alianza elimu ya Sekondari mwaka 2002 nakuhitimu mwaka 2005 katika shule ya Luhuiko mjini Songera,baada ya hapo aliamia jijini Dar es Salaam na kujiunga na Chuo cha Sanaa cha Kaole mjini Bagamoyo mwaka 2006 na kuhitimu masomo yake mwaka 2007”alisema Salumu Kilowoko. 

Alisema kwamba, familia iliamua kumpeleka marehemu katika chuo hicho kwa sababu walibaini kwamba alikuwa na kipaji cha uigizaji tangu akiwa mdogo, lakini kwakuwa alikuwa kijijini kibaji chake akikuweza kufahamika mara moja kwa watanzania.

Marehemu Sajuki alianza kujulikana katika tasnia ya filamu nchini mwaka 2008, baada ya kutoa filamu ya Mboni Yangu waliofanya na mkewake Wastara Juma Kilowoko, ikafuatiwa na Two Brothers na Vitamkonaye zote akiwa na mkewe Wastara.

Mapenzi ya Wastara na Sajuki yalianza baada ya wawili hawa kukutanishwa na msanii mwenzao Deugratius Shija, wakati wa kuandaa Movie ambayo akuitaja mara moja kwani marehemu na Wastara hawakuwa wanajuana kabla.


" Mipango ya kumtafuta msichana tutakaye igizanaye kwenye movie yetu ndio chanzo cha wawili hawa kujuana na maisha yao ya mapenzi yakaanzia pale mpaka hivi sasa amefikwa na umauti" Alisema Shija

Sajuki pamoja na Wastara katika mafanikio yao kwenye tasnia ya Filamu, walibarikiwa kuanzisha kampuni inayokwenda kwa jina la Wajey Film Production mwaka 2008, ambayo ni muunganiko wa majina yao. Mpaka anafikwa na umauti Sajuki ameacha mke na mtoto mmoja wa miezi10

Sajuki alianza sanaa katika kundi la jumba la dhahabu kabla ya kuanza kuandaa filamu zake mwenyewe kupitia Kampuni yake ya Wajey Filam Production na mpaka mauti yanampata alikuwa na filamu saba huku ya nane ikiwa sokoni na itaanza kuonekana wiki ijayo.

posted on 4.Jan.2013
by: Loyce Joseph 

*******************************************************

HISTORIA YA BOXING DAY, NA UTOFAUTI WAKE KWA BAADHI YA MATAIFA DUNIANI



Mpaka hivi leo neno BOXING day bado halijatafutiwa maana yake (unclear).Kuna tafsiri tofauti ya siku hii ulimwengu mzima, wengi husema Boxing Day ni muda wakuspend au chill out na ndugu na marafiki, usually wale ambao hamjaonana siku ya Xmas yenyewe, au siku ya kuweka mashindano maalum ya kupigana.

Ila Katika utamaduni wa Ulaya, wao wanaamini Boxing day ni siku ya kutoa msaada kama vile pesa au zawadi kwa wale wasiojiweza, makundi maalum kama walemavu, watoto yatima NK. Romania wao walikua wakiandaa zawadi nakuzipack kwenye maboksi siku kama hii nakuzipeleka katika makanisa mbali mbali. Kwaiyo Boxing day ni holiday tu kama nyingine ila utofauti wake nikwamba siku hii inasheherekewa siku moja baada ya Christmas.

Kwenye nchi za Ulaya, Canada, Australia au New Zealand wanachukulia Boxing Day kama siku ya kufanya shopping, yani (shopping holiday), ambayo siku hii kwa upande wa Marekani ni siku baada ya Thanksgiving (Black Friday).

Boxing Day in the UK na baadhi ya maeneo Marekani ni siku ya wawindaji mbwa mwitu(Fox).Ata baada yakuzuiliwa kwa Uwindaji wa Fox Ulaya na sheria ya uwindaji wa 2004 (hunting act),Boxing Day imebakia kuwa siku kubwa sana kwa wawindaji wa mbwa mwitu huko Ulaya.

Katika baadhi ya nchi barani Afrika kama,  Commonwealth nations, particularly Ghana, Uganda, Malawi, Zambia and Tanzania, prize fighting contests are held on Boxing Day. This practice has also been followed for decades in Guyana and Italy., Nchi nyingie huadhimisha Boxing day kwa staili hiyo ya kuandaa mashindano ya nguni

Mpaka hizi sasa Nchini Tanzania kuna utaratibu wa kupeana zawadi ambao maranyingi hufanywa na watu wenye mahusiano ya kimapenzi, marachache sana kwafamilia zao kupeana zawadi au kuwapelekea watu wasiojiweza


Posted on 26.12.2012
By: Loyce Joseph

***********************************************************************************
TUKIO LA KUPIGWA,KUTESWA NA KUUMIZWA KWA RAISI WA MADAKTARI NCHINI. Dr. STEVEN ULIMBOKA, AMBALO LILITOKEA JUNE 27, 2012. NI MIONGONI MWA MATUKIO AMBAYO YAMEACHA HISTORIA KWA MWAKA 2012

PICHA TATU ZA STEVEN ULIMBOKA KABLA YA KUPATWA NA KADHIA HIYO



Dr.Steven Ulimboka Baada ya kufikishwa Hospitali ya Muhimbili kwa matibabu, kutokana na tukio la kutekwa na watu wasio julikana na kufanyia ukatili wa kutisha

                                  *****************
BAADA ya kupata matibabu,Dr.Steven Ulimboka alirejea nchini akitokea Afrika ya Kusini, nakupokelewa na Ndugu Jamaa na Marafiki

                                                    **********************
Magazeti nayo yalitoka na vichwa vya Habari mbalimbali, juu ya tukio hilo, kwa jinsi lilivyo tikisa kwa hisia mbalimbali


  ****************************************************************************

ZIJUE ATHARI ZA MADINI YA URANIUM,KWA NINI UCHIMBAJI  WAKE    WAZUA UTATA NCHINI, NINI KIFANYIKE
madini ya URANIUM

Tanzania nimiongoni mwa nchi za Afrika zilizo jaliwa rasilimali ya Madini, ikiwa na aina 8 za madini ambazo nazo zina aina nyingine za madini ndani yake ikiwemo TANZANITE ambayo aipatikani malipopote duniani isipokuwa Tanzania, kitu ambacho kina kamilisha kuwepo kwa idadi kubwa ya madini tofauti tofauti.Aina hizo za madini ni Diamonds, Gold, Base Mentals na PGM, Ferrous Mental, Tin- Tungsten, Gemstones, Carbonates, Coal na hivi sasa kuna Uranium.ilikupata ufahamu zaidi tembelea tovuti ya www.tanzania.go.tz/mining.html

Hivi karibunu Serikali ilitangaza kuanzishwa kwa mradi wa kuchimbwa kwa madini ya URANIUM, katika kijiji cha Bahi huko Dodoma na maeneo mengine. Uchimbwaji wa madini haya umekuwa ukipigiwa kelele na baadhi ya Wanaharakati pamoja na kituo cha Haki za Binadamu Legal Human Right Centre (LHRC).

Kwamujibu wa kijarida kilicho chapishwa na shirika hilo, kinaelezea juu ya madhara ya kimazingira kiafya na kiuchumi kwa Taifa letu, endapo tutaendelea nania ya uchimbaji wa madini hayo

Madini ya Uranium nimadini yenye mionzi, yakiwa na uzito na ujazo mkubwa.pia yamegawanyik katika seemu kuu sita,ila yana fanya kazi katika seemu kuu mbili U-238 na U-235,nakatika hizo njia mbili kuna mionzi aina ya ALFA,GAMMA na BETTA ambayo husababisha adhari kwa manadamu

Uranium hutumika, kutengeneza Silaha hatari za Nyuklia pamoja na uzalishaji wa Nishati ya Umeme,ilikupata umeme madini haya yanarutubishwa mpaka kufikia kipimo cha Isotopes-235. Uzalishaji wa umeme kutumia madini haya huitaji tahadhari kubwa ya kimazingira.

Kwa upande mwingine Miss Rachel Juma Chagonja ambaye ni Co-Ordinator, kutoka kituo cha Civil Education is the Solution for Environmental Management- CESOPE. Amesema serikali ya Tanzania inajua madhara yaletwayo na madini haya, kutokana na tafiti iliyo fanywa na shirika hilo mwaka 2009 katika eneo la Bahi Mkoani Dodoma, yenye lnego lakuonyesha faida na hasara za madini hayo

picha ya Isotopes-23
Miss Rachel Chagonja anasema, Kulingana na kipato cha madini hayo ambayo inakadiriwa kuwa Billioni 200 na zaidi kwa miaka 12, haina faida, ukilinganisha na madini mengine yanayo patikana nchini.
kwamantiki hiyo shuguli zingine za kibiashara ambazo hufanywa na wananchi zinafaida kuliko madini hayo.Alisema Rachel.

Madhara yake huweza kumuingia mtu,kupitia Kuvuta hewa lenye Vumbi ya Uranium, Kunywa maji yenye mionzi yake, kupungua kwa uwezo wa kutunga mimba na kupata mtoto kwa wanaume na wanawake.kuzaa watoto wenye upungufu kiakili na kwenye maumbile kama ulemavu.pamoja na Ugonjwa wa CANCER

Katika Mazingira, Rachel Chagonja amesema, viumbe hai uadhirika sana, kutokana na maji yanayo tiririka kutoka katika migodi hiyo, ambayo hutumiwa na mifugo na binadamu, uharibifu wa ardhi kutokana na mashimo.

Uchimbaji wa madini haya pia uchangia tatizo la upatikanaji wa maji safi duniani, mfano tukio la Fukushima nchini Japan ambako vinu vya Nyuklia vilipasuka na kusababisha maji ya eneo hilo kuwa sumu kwa matumizi ya mwanadamu.Alisema Rachel Chagonja

Katika swala la Migogoro na historia ya Vita kwenye nchi ambazo madini haya upatikana, Alisema Tanzania inapaswa kuwa makini nakuepuka kufanya maamuzi yenye malslahi ya watu wachache, pia nimuhimu kutoa elimu kwa wananchi ili waweze kutoa idhini na maamuzi ya maendeleo ya Taifa lao.Alimalizia Rachel Chagonja

.......................................................................................................................................................

      JE TUNA WAKUMBUKA WALEMAVU


Leo ni siku ya walemavu Duniani, kama taifa linalo jali na kujua matatizo na changa moto juu ya kundihili maalum katika jamii yetu.Taifa imeandaa maadhimisho ambayo yanafanyika leo Mkoani Mara ili walemavu wapate fursa ya kusema maitaji yao kwa jamii.Kaulimbiu ni ONDOA vIKWAZO TUJENGE JAMII SHIRIKISHI KWA WOTE.

Question is:
             Taratibu ambayo inafanywa na serikali pamoja na wadau wengine, hasa katika siku ya maadhimisho
             tu, nakujisaau katika siku ziungine juu ya matatizo ya Walemavu..Je inatosha katika kutatua maitaji
             ya walemavu?

              Taratibu za jamii au familia zetu kuwa tumia walemavu kama kitega uchumi na kuwapeleka maeneo
              ya barabarani na kuombaomba ni sahihi?

              Familia na jamii zetu, zinafanya jitihada ya kuwasaidia walemavu au unyanyapaa ndio unao
              ongoza katika kutoa maitaji yao?
   
              Kutokuwepo kwa alama na miundombinu ambayo inawasaidia walemavu kufanya shugulizao kama
              watu wengine inaonyesha kutoshirikishwa na Taifa katika shuguliza uzalishajii



Ongea na jamii kupitia Campus Vision, ilikuweza kutoa ninjia gani sahihi ambayo jamii yetu inapaswa kufanya ilikuwasaidia Walemavu.
                             Coment yako nimuhimu:

1 comments:

jamii inatakiwa kujua kuwa walemavu wanaitaji msaada wetu nasio kuwa bagua na kuwaficha ndani..tuamke tanzania

New comments are not allowed.