Tuesday, June 18, 2013

WABUNGE 4 WA CHADEMA NA WANANCHI 60 NA MIKONONI MWA POLISI, MHE MBOWE, TUNDU LISU HAWAJULIKANI WALIPO




Jeshi la polisi  mkoani Arusha limewakamata wabunge 4 wa chadema ambao majina yao hayajajulikana mara moja, pamoja na wananchi wengine wapatao 60 huku msemaji wa kambi rasmi ya upinzani Mhe. Freeman Mbow pamoja na Mbunge wa Singida mjini Mhe. Tundu Lisu wakiwa hawajulikani walipo baada ya polisi kutawanya wafuasi wa chama hicho

Wanachama hao walijikusanya katika uwanja wa Soweto mkoani humo wakiwaaga wale waliouwawa na Bomu hapo Juzi ambapo Polisi ilidai kuwa ni kukusanyika eneo la soweto bila kibali cha sertikali

Kwa habari ambayo Blog hii imeipata kutoka kwa shuhuda huko Arusha nikuwa hali bado ni tete na kuwa kuna majeruhi kadhaa wamekimbizwa katika Hospitali ya mount Meru kwa matibabu zaidi juu ya tukio hilo

Utapata Updates kadri tutakavyokuwa tunazipata 





Chama cha Demokrasia na maendeleo CHADEMA kimeichukuliwa hatua ya serikali ya kutangaza dau la shilingi Mil. 100 kwa yeyote atakaye fichua taarifa za kumtia hatia aliye husika na tukio la kurusha bomu lililo sababisha vifo vya watu 4 nakuacha wengine 50 wakiwa wamejeruhiwa vibaya

Hatua hiyo iliyopingwa na Chadema ilitangaza jana Bungeni Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Uratibu na Bunge Mh. Willium Lukuvi ambapo Mkurugenzi wa habari na mawasiliano Mhe. John Mnyika amesema kitendo hicho nikutumia vibaya fedha na rasilimali za serikali

Akiongea hii leo jijini Dar es salaam katika makao makuu ya chama hicho, Mhe. Mnyika amesema fedha hizo ambazo serikali imezitangaza Ingekuwa bora kama wangezitumia kuwa fariji majeruhi na waliopoteza ndugu zao katika tukio hillo, amesema Mnyika

Mnyika amesema, chama hicho kimetoa Baraka zote kwa wabunge wake kutohudhuria Bungeni mpaka pale maombolezo yatakapo malizika huko Arusha na kwamba Mbunge yeyote wachama hicho hataruhusiwa kuhudhuria Bungeni

Aidha Mhe. Mnyika ameongeza kuwa chama hicho kimesikitishwa na kitendo cha Bunge kutositisha shuguli zake kutokana na tatizo la Arusha wakati majanga kama haya yanapotokea kwani kwa mujibu wa kanuni za Bunge inaruhusiwa kusimamisha shuguli zote mpaka hali ikae sawa.

“Bunge linatumiwa na serikali kuchamazisha haki, Polisi nao wanatumika na Serikali lakini ukweli ni kwamba bado tuna muhimili wa mahakama ambayo naamini yenyewe itasimamia haki daima”alisema Mnyika.

Kuusiana na mkanda wa video ambao chama hicho inadai inamuonyesha Polisi wa kikosi cha FFU akilipua bomu hilo, Mnyika amesema watasubiri mkanda huo kupitiwa na mwanasheria kwanza na viongozi wengine wajuu wa chama hicho iliwaweze kuitoa kwa wananchi wote kuiona

“Mkanda tunao na ushahidi hupo, tusubiri taratibu za kuupitia ilituweze kuangalia hasara na faida za kuutoa kama tutaona inafaa ama laa kila mtu hatauona mkanda huo”Alisema

Chama cha CCM na CHADEMA vimekuwa vikitupiana lawama kutokana na vifo vya watu 4 vilivyo sababishwa na kulipuka kwa bomu huko eneo la Soweto, jeshi la polisi likiwa kiwa limeunda kamati kuchunguza tukio hilo

WATOTO WAOMBA SIKU YAO KUJADILI RASIMU, LHRC NAO WAZIDI KUJITOSA KUTETEA HAKI ZAO



Kituo cha sheria na haki za binadamu, hii leo kimefanya maadhimisho yake ya siku ya mtoto wa Afrika katika viwanja vya posta kijitonyama jijini Dar es salaam wakiwa na kaulimbiu isemayo Kupinga tamaduni na mienendo hasi dhidi ya watoto ni wajibu wa jamii nzima

Akionge na waandishi wa habari katika maadhimisho hayo, Mkurugenzi mkuu wa kituo hicho Bi Helen Kijo Bisimba amesema kuwa, pamoja na kuwa wameshiriki katika mchakato wa kuhimiza haki za watoto katika katiba mpya lakini wamefurahi kuwa watoto wengi sasa wanauelewa juu ya siku hiyo pamoja na haki zao.

“ Watoto wengi sasa wanaelewa umuhimu wa siku hii, pamoja na jitihada zetu tunaamini kunamafanikio yatafikiwa, kuanzia ndani ya Rasimu na katiba yenyewe” alisema Hellen


Aidha Kamishna msaidizi wa wizara ya Afya na ustawi wa jamii bwana Rabikira Mushi amesema, ni wakati sasa kwa jamii nzima kutambua suala la kulinda haki za watoto ni la jamii nzima na kwamba kila halmashauri ina wajibu wa kulinda haki za watoto katika maeneo yao.

“Halmashauri zote zinatakiwa kujali watoto kwenye maeneo yao bila kujali huyu ni mzaliwa wa hapo au nimgeni kwani jukumu la watoto nilakwao kisheria na sio ombi, pamoja na jamii nayo itambue hilo sio kuwaachia serikali tu nilazima kila mtu ajiwajibishe juu ya kulinda haki za watoto” Alisema Rabikira

Miongoni mwa watoto waliohudhuria maadhimisho hayo kutoka shule mbalimbali,Blo hii ilipata fursa ya kuongea na Aneth George kutoka Kibasila Sekondari pamoja na Adnan Kaizer kutoka
Makongo Sekondari wakielezea jinsi gani wameipokea siku hiyo na mapendekezo yao kwa jamii juu ya haki za watoto


Aneth alisema, Hakizao nilazima zilindwe na kuwa Serikali iteuwe siku moja kwa watoto kujadili haki zao ndani ya Rasimu ya katiba mpya ilinao wajue hakizao zitakazo kuwepo katika kabita mpya. Alisema Aneth

Adnan Kaizer kwa upande wake amesema, suala la wazazi hasa wa kambo kuwatumikisha watoto kinyume na uwezo wao na sheria isemavyo sio haki nakuwa kila mtu awajibike kumlinda mtoto. Aslisema Adnan

Siku ya mtoto wa Afrika huadhimishwa kila mwaka Duniani kote, tarehe 16 June lakini shirika la LHRC limeamua kufanya hii leo. Kimataifa shirika la Kazi Duniani ILO lilitoa ripoti yake kuhusiana na siku hiyo ambapo watoto Milioni 10.5 barani Afrika wanatumikishwa majumbani

Monday, June 17, 2013

MLIPUKO ARUSHA, SERIKALI KUTOA MILIONI 100 KUMPATA MTUHUMIWA



Huku watanzania wakiwa katika hali ya sinto fahamu kutokana na bomu lililolipuka huko Arusha na kujeruhi watu zaidi ya 55 huku watu 3 wakiwa wamefariki hadi hivi sasa kutokana na Bomu hilo



Tayari Serikali imeunda tume kuchunguza tukio hilo, pamoja na kutoa kiasi cha Shulingi Millioni 100 kwa mtu yeyote atakaye toa taarifa za kumkamata mtu ambaye anahusika na tukio hilo ilihatua zaidi ziweze kuchukuliwa



Akiongea mapema leo Bungeni,Waziri wa nchi, ofisi ya waziri mkuu sera na uratibu wa Bunge Mhe. William Lukuvi amesema serikali itatoa jumla ya shilingi Milioni 100 kwa yeyote atakaye mtaja aliyehusika na tukio hilo huku akiwasihi watanzania kuwa wamoja na kutokubali kutumiwa na watuwasio kuwa na mema kwa Taifa letu

Thursday, June 13, 2013

TAMASHA LA FILAMU NCHINI KUANZA JULAI MOSI 2013 MKOANI MWANZA

Tamasha la Filamu nchini lijulikanalo kama Tanzania Open Film linatarajia kufanyika katika jiji la Mwanza kuanzia Julai mosi mpaka Julai 7 mwaka huu





Akizungumza kwa niaba ya wasanii wenzake Muigizaji Jacob Steven maarufu kama JB amesema hiyo ni nasafi kubwa sana kwa wasanii kwa sababu watapata fursa ya kuonana na mashabiki wao na kuzungumza nao moja kwa moja,


Pia watatumia nafasi hiyo kugawa vyandarua katika Hospitali ya sekoture iliyopo jijini Mwanza ilikuweza kuwasaidia akina mama na watoto katika hospitali hiyo


Meneja wa Habari na mawasiliano wa TBL Edith Mushi amesema, katika miaka miwili iliyopita tangu tamasha hilo kuanza wamejifunza vitu vingi sana kikubwa nikuwa watanzania wengi wanazipenda na kuzikubali Filamu za kitanzania

Aidha Edith, amesema wanaendelea kushirikiana na Sophia Records kuandaa tamasha hilo, Ambapo Mkurugenzi wa kampuni ya Sophia Records bwana Mussa Kissoky amesema waliamua kuanzisha tamasha hilo baada ya kuona kiu ya watanzania kupata fursa ya kukutana na wasanii wao


Hatahivyo, ilifahamika kuwa kutokana na hali yakuwa na vurugu za hapa na pale Tamashahili lilitakiwa kuwa mkoani humo na badala yake likapelekwa mkoani Mwanza


Wednesday, June 12, 2013

KESI YA BALOZI MZENGI NA BIASHARA YA KUSAFIRISH MWANADAMU, YAHUSISHWA ZIARA YA OBAMA NCHINI TANZANIA

Licha y Balozi wa Marekani nchini Tanzania, Alfonso Lenhard kutoa sababu ya ziara ya Rais wa Taifa la Marekani, Barack Obama nchini Tanzania haina ajenda ya siri: "kuna maswali mengi naulizwa kwa  nini Rais Obama amechagua kuzuru Tanzania.

Balozi Lenhardt alisema: kuwa"Ni kweli Obama atakuja Tanzania. Lakini niwahakikishie tu kuwa haji kupora rasilimali za Tanzania, huku akitaj sababu nne ambazo ni kutokana na kuwa Tanzania ni mfano wa utawala bora, demokrasia na ushirikishaji wa watu wake wakati wa kufanya uamuzi unaogusa maisha yao ya kila siku. Akasema Tanzania ni nchi ya mfano linapokuja suala la uongozi bora na ndiyo maana imekuwa na amani na utulivu kwa muda mrefu ikilinganishwa na nchi nyingi za Kusini mwa Jangwa la Sahara: 

 
“Rais Obama anakuja kuunga mkono juhudi za Watanzania katika kutengeneza mazuri ya uwekezaji lakini bila kusahau kuwa kasi ya ukuaji wa uchumi wa Tanzania imeivutia Serikali ya Marekani.”
Kuisaidia Tanzania kuendeleza fursa mbalimbali za kujiletea maendeleo. Alisema uendelezaji huo wa fursa una lengo la kuisaidia Serikali ya Tanzania kukabiliana na tatizo la umaskini na kwamba Marekani ni moja ya nchi zinazoongoza kwa kutoa fedha nyingi za misaada na akisema kwa mfano, mwaka 2012 pekee ilitoa Dola 750 milioni. 

Kuhimiza haja ya Afrika kutayarisha viongozi wa kizazi kijacho. Ameanzisha programu ya kuandaa viongozi wa kizazi inayoitwa `Young African Leaders Initiative’ na Watanzania watatu, Modesta Lilian Mahiga, Masoud Salim Mohamed na Malula Hassan Nkanyemka walishiriki katika mpango huo na kukutana na kiongozi huyo mwaka 2010: 

Hayayote hayaja waridhisha wachambuzi mbalimbali wa kiasi huku kila mtu kuamini ajuavyo na kwa muono wake yeye,  katika uchambuzi wa Tovuti ya Washington Post huko mrekani mchmbuzi mmoj hajaridhishwa na ziara ya Ris huyo nchini Tanzania huku akiilingnish Tanzania na nchi inyotetea biashara ya binadamu (
 human trafficking. ) kwa kufananisha  tukio alilolifanya blozi wa Tanzani huko Washington bwana Allan S Mzengi dhidi ya  Zipora Mzengo 


Kusoma alichokiandika Dana Milbaank ktika tovuti ya The Washington Post juu y Rais Obama Kuja Tanzania Fungua hap chini kusom zaidi 

http://www.washingtonpost.com/opinions/dana-milbank-obamas-ill-advised-visit-to-tanzania/2013/06/07/397b00fa-cf88-11e2-8845-d970ccb04497_story.html


LORI AINA YA SCANIA LATEKETEA KWA MOTO MBEZI

Jana Majira ya saambili usiku meneo ya Mbezi beach samaki Lori aina ya Scania lenye namba za usajili T 194 ATR liliungua moto kutokana na tairi la mbele kupata pancha likitokea maeneo ya tegeta

Moto huo uiliteketez eneo lote la mbele laa gari hilo ambalo lilikuwa limebeba mchanga, Kwmujibu w Meja Nurdin mkuu wa kituo cha polisi cha Afrikana, Gari hilo linamilikiwa na kmpuni ya Kilimanjaro Track.


Kikosi cha zima moto kilifika eneo la tukio nakufanikiwa kuzima moto huo kabla gari hilo alija sababisha madharaa makubwa,

Chajabu nikwamba licha yaa wnanchi kuona moto huo ukiwak kwa kasi lakini bado walijazana eneo la tukio huku madereva nao wakikatiza pembeni kabisa ya gari hilo lililokuwa likiendelea kutekete kwa moto

Katika tukio hilo hakuna mtu yeyote aliye ripotiwa kupoteza maisha.