RAIS KIKWETE: Kampeni za Uraid hazijaanza rasmi, Amtaka Philip Mangula Kuwashugulikia wanao fanya kampeni

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM), Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete amesema kuwa kampeni za kugombea kuteuliwa kuwa mgombea urais wa Tanzania kupitia Chama cha Mapinduzi (CCM) hazijaanza rasmi.
 
Aidha, Rais Kikwete amesema kuwa vitendo vya baadhi ya watu kuanza kampeni kabla ya wakati wake ni moja ya mambo yanayosikitisha.

Hata hivyo, Rais Kikwete amesema kuwa suala hilo zima limekabidhiwa kwa Makamu wa Mwenyekiti wa CCM (Tanzania Bara) Mzee Philip Mangula ambaye atalisimamia jambo hilo na kulishughulikia.

Rais na Mwenyekiti wa CCM alikuwa anazunguza na wajumbe wa Halmashauri ya CCM ya Mkoa wa Mbeya kwenye Ukumbi wa CCM mjini Mbeya.katika ziara ya kikazi ya siku mbili mkoani Mbeya.

Maandalizi Bunge La Katiba, Rais akagua Ukumbi wa Bunge Dodoma

Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete leo, Jumamosi, Februari Mosi, 2014, amekagua na kuridhishwa na kazi na kasi ya marekebisho yanayofanywa katika Ukumbi wa Bunge mjini Dodoma ikiwa ni maandalizi ya Vikao vya Bunge Maalum la Katiba linaloanza baadaye mwezi huu.

Rais Kikwete amesimama kwa muda mjini Dodoma kujiridhisha na mwenendo wa maandalizi ya Bunge Maalum akiwa njiani kwenda Mbeya ambako atafanya ziara ya kikazi ya siku mbili.

Rais Kikwete amekagua Ukumbi huo na huduma nyingine muhimu kwa ajili ya vikao hivyo ikiwa ni pamoja na bwalo la chakula kwa kiasi cha dakika 45 na kuvutiwa na mwenendo wa kazi na kasi ya marekebisho kwenye ukumbi huo.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Mheshimiwa William Lukuvi amemhakikishia Rais Kikwete kuwa kazi yote ya kufunga viti na vipaza sauti, ambavyo vitatumia mfumo wa kisasa wa mawasiliano ya kadi, ndani ya ukumbi huo itakuwa imekamilika ifikapo Februari 10, mwaka huu, siku tisa kuanzia sasa.

Bunge Maalum litakuwa na wajumbe 645 ambao ni Wabunge wa sasa wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Wajumbe wa Baraza la Wawakilishi la Zanzibar na Wajumbe 201 ambao watateuliwa na Rais kutokana na mapendekezo ya makundi mbali ambayo yanatajwa katika Sheria ya Marekebisho ya Katiba.


EmoticonEmoticon