WATU WANNE WAKAMATWA KWA KUNUNUA KADI YA MPIGA KURA MOROGORO



Ikiwa imebaki siku chache kuelekea uchaguzi mkuu katika hali isiyo ya kawaida watu wanne wasiofahamika itikadi zao za kisiasa  wamekamatwa na wafuasi wa chama cha demokrasia na maendeleo(chadema) kwa madai ya kupita katika kata za manispaa ya morogoro na kudai shahada za wapiga kura kwa nguvu na kuanza kuorodhesha majina ya wananchi na namba zao za simu




kwa upande  wananchi mashuhududa   waliokumbana na watu hao  katika harakati za  kuwaandikisha  wapiga kura majina  wameeleza jinsi watu hao walivyokuwa wakifanya zoezi hilo  kwa kudai kwa lazima shahada za kupigia kura ambapo baadhi ya watu  walikubali na wengine wafikisha  jambo hilo kwa afisa mtendaji wakata na wananchi waliamua kuungana na kuwakamata na kisha kuwapeleka katika kituo cha polisi cha mji wa morogoro.



Akitolea ufafanuzi kuhusiana na suala hilo msimamizi wa uchaguzi jimbo la  morogoro mjini  bi theresia mahongo amesema kuwa kufanya hivyo ni kosa la jinai na kwamba adhabu yake ni faini kati ya shilingi laki moja hadi laki mbili au kifungo cha miaka miwili ama vyote na kuwaonya wananchi kuacha kufanya hivyo nikosa la jinai



EmoticonEmoticon