MAJINA YA WANAFUNZI WALIOJIUNGA NA KIDATO CHA TANO/VYUO KUTANGAZWA LEO




Naibu Waziri wa Elimu Mhe. Filipo Mulugo Asubuhi hii anatarajia kutangaza majina ya wanafunzi walio chaguliwa kujiunga na kidato cha tano pamoja na wale watakao jiunga na vyuo vya ualimu na ufundi

Majina yakupangiwa shule pamoja na vyuo yamechelewa sana tofauti na ilivyo zoeleka, kwani kwa taratibu za awali majina hayo hutangazwa mwezi wa tano ikiwa ni miezi miwili kabla ya kufungua shule ili kutoa nafasi kwa wazazi na wanafunzi kujiandaa na kujiunga na masomo yao

Katika hali isiyo yakawaida majina hayo yata tangazwa hii leo ikiwa tayari shule zimefunguliwa huku waliingia kidato cha sita wakianza masomo yao huku kukiwa hakuna wanafunzi wa kidato cha sita

Endapo shule itakuwa imefungua ikiwa na wanafunzi wa kidato cha tano basi pia itakuwa maajabu mengi juu ya mfumo wa elimu, Ikumbukwe kwamba matokeo ya wanafunzi hawa kwa mwaka 2012 yalitikisha nchi kutokana na asilimia 80 yawanafunzi kufeli vibaya huku idadi ya wanafunzi wachache ndio walifaulu.

Kutokana na hali hiyo Waziri Mkuu wa Tanzania Mhe. Mizengo Pinda alilazimika kuunda tume ya kuchunguza sasabu za kufeli kwa wanafunzi hao na baadae ikapatikana pendekezo la kufanya standardization ili kuweza kuoka idadi kubwa ya wanafunzi waliofeli na baadae matokeo kutangazwa upya

Hata hivyo baada ya Standardization kufanyika ilitegemewa kuwa wizara itatoa taarifa ya kutangaza ni wali na lini wanafunzi watajiunga na masomo yao ya kidato cha tano kwa wale waliofaulu kwa vyuo na kidato cha nne


Habari zinazo husiana

Bonyeza hapa chini ili kusoma zaidi juu ya matokeo ya kidato cha nne 2012 tangu kutangazwa mpaka hii leo



Habari kamili itakujia hapa hapa .....................

1 comments:

Kwa muda uliobaki jamani tutajiandaaje hasa sisi wazazi na kama mtoto wako ulikwisha mpeleka shule inakuwaje??


EmoticonEmoticon