WASANII WAKUTANA LEADERS CLUB KUJADILI MAZISHI YA MANGWAIR


Marehemu Ngwair akiwa na msanii M2 the P huko Afrika kusini kabla ya kufikwa na umauti

Baadhi ya wasanii wamekutana jioni hii ilikujadili jinsi ya kumpumzisha msanii mwenzao nguli Albert Mangwair, wasanii hao wako katika viwanja vya leaders club
Tayari kamati ya wakongwe wa muziki wamepanga kamati ya mazishi ambayo itaongozwa na Lady Jay Dee, Prof Jay, Mchizi mox, Nura, Pre Funk majani na
NURA AKANA MANGWAIR KUTUMIA MADAWA YA KULEVYA
Msanii Nura alipohojiwa na kituo cha EATV kuusu arehemu kutumia madawa ya kulevya amekana kujua swala hilo na kuwa hajawahi kumshuhudia marehemu akitumia madawa hayo
“Sijawahi kumshuhudia ngwair akitumia madawa licha ya kusikia watu wakisema sana kuusu hilo, kama unavyo jua wabongo wanaongea sana hivyo kujua kitu cha ukweli au uongo nivigumu” Alisema Nura na kutoa masikitiko yake juu ya kifo hicho

HISTORIA YA MAREHEMU, MANGWAIR
Jina lake kamili ni Albert Keneth Mangwair, ni mzaliwa wa Ruvuma kwa kabila ni Mngoni wa kutoka Songea. Mangwair alizaliwa mkoani Mbeya mnamo tarehe 16 Novemba mwaka 1982 akiwa ni mtoto wa mwisho katika familia ya watoto 10, lakini katika uzao wa mama yake mzazi yeye ni motto wa 6.
Baada ya kufikisha miaka 5, Mangwair alihamia mkoani morogoro kwaajili ya kuanza shule ya msingi ya Bungo iliyopo hukohuko Morogoro, lakini baadae walihamia mkoani Dodoma ambako alimalizia masomo yake ya helium ya msingi.
Baadae alifanikiwa kujiunga na shule ya sekondari Mazengo kasha kuendelea na elimu ya chuo katika chuo cha ufundi Mazengo, Kwaufupi alianza kuimba tangu akiwa mdogo mpaka hapo nyota yake ilipo gara kwa watanzania.

MAZISHI KUFANYIKA MKOANI MOROGORO
Wapendwa wa karibu na mashabiki wote wakiwa wanasubiri kuwasili kwa mwili wa mpendwa wetu kutoka huko Afrika kusini aliko patwa na umauti
Kwa mujibu wa baba mdogo wa marehemu, mzee Mangwair ambaye yuko mbinga songea amesema kuwa wamekubaliana na kaka yake mkubwa yani baba mkubwa wa Mangwair David Ngwair, kuwa watakutanika Mbezi kwa msiba na pia mapokezi yatafanyika hapa Dar es salaam.
Mazishi yatafanyika mkoani Morogoro mahali alipozikwa baba mzazi wa msanii Mangwair.

MSANII ALIYEKUWA NAYE YUKO MAHUTUTI
Msanii aliyeongozana na mangwair ambaye anafahamika kwa jina la M to the P, Naye aliyake haiku zivuri na taarifa zinasema kuwa anapumulia mashine na manesi wanasema amelishwa kitu kinacho sadikiwa kuwa ni sumu nab ado anapat matibabu hukohuko Afrika ya kusini


EmoticonEmoticon