KUELEKEA BAJETI YA WIZARA YA ELIMU NA MAFUNZO YA UFUNDI WALIMU WAPAZA SAUTI, WALIA SERIKALI KUZIDI KUWAPUUZA


Chama cha walimu Tanzania kimeitaka jamii kutambua kuwa mgogoro kati ya walimu na serikali bado upo palepale kutokana na serikali kutokubali kutekeleza madai ya walimu kwa kiwango wanachohitaji.

Akiongea leo jijini Dar es salaam, Rais wa chama cha walimu Tanzania Bw. Gratian Mukoba amesema wabunge watakapokuwa wakijadili bajeti ya wizara ya elimu wiki ijayo watambue kuwa mgoggoro huo bado upo.

Serikali itambue bado hatuja kubaliana juu ya madai yetu, hivyo mgogoro bado hupo pia wabunge watambue hilo ili serikali ijadiliane juu ya maslahi ya walimu” Alisema Mukoba

Aidha CWT iliamua kukubaliana na serikali kufanya majadiliano kwa faida ya walimu na ustawi wa elimu katika kikao cha baraza la majadiliano ambacho kilifanyika Mjini Morogoro tarehe 09 mpaka 10/12013 na tukakubaliana kufanya kikao kingine Februari 2013

Katika kikao hicho tulitaka ongezeko la mishahara,posho kuongezeka kwa asilimia 30 na asilimia 50 kwa walimu wa sanaa na walimu wa sayansi asilimia 50 tu, lakini serikli haikutimiza hayo” alisema

CWT ilipeleka mchanganuo unaopelekea uhalali wa madai yake, serikali ilitakiwa kushugulikia madai hayo haraka kabla ya kuitishwa kwa kikao kingine cha majadiliano na baadae CWT ilitimiza jukumu lake kwa kukubidhi serikali Justification yake tarehe 06/02/2013 lakini serikali ilikaa kimya. Alisema Mukoba

Tulikaa tena tarehe 21/03/2013 hukohuko Morogoro lakini serikali haikuja na yale tuliyo hitaji nabadala yake iliripoti kuwa mchakato wa ufuatiliaji offer bado unaendelea jambo ambalo halikuturidhisha” Alisema Mukoba
CWT waliomba fursa ya kumwona waziri wa elimu na mafunzo ya ufundi kupitia, mwenyekiti, makamu mwenyekiti na katibu wa baraza ambapo tarehe 24 mpaka 25/05/2013 majadilihao hayo yalifanyika jijini Dar es salaam. Alisema Mukoba

katika kikao hicho, walihitaji Ongezeko mishahara kwa asilimi 100, posho ya kuundishia (Teachers allowance) 55% kwa walimu wa sayansi na 50% kwa walimu wa sanaa, posho ya 30% kwa walimu wanaofanyakazi katika mazingira magumu. Mambo ambayo walitaka wabunge watambue kuwa bado hayajatatuliwa

Hivyo CWT imeitaka serikali kuwa na nia njema na ikubali kurudisha mioyo ya walimu iliyokufa kwa kukata tamaa ilikufufua utendaji wao na kuboresha elimu ya Tanzania.

Bajeti ya mapato na matumizi ya mwaka wa fedha 2013/2014 kwa wizara ya elimu na mafunzo ya ufundi inatarajiwa kusomwa mapema wiki ijayo huko Bungeni Dodoma


EmoticonEmoticon